Star Tv
 
 

Mkuu mpya wa baraza la kijeshi mpito nchini Sudan amesema leo kuwa serikali ya kiraia itaundwa baada ya mashauriano na makundi ya upinzani na kuahidi kuwa kipindi cha mpito kitadumu kwa muda usiozidi miaka miwili.

Wakati wa hotuba yake ya kwanza kwa njia ya televisheni Jenerali Abdel Fattah al-Burhan ametangaza pia kuondoa marufuku ya kutembea usiku na kuamuru kuachiwa huru kwa watu wote waliofungwa chini ya sheria ya hali ya hatari iliyowekwa na utawala ulioangushwa. Wakati huo huo mkuu wa idara ya ulinzi na ujasusi nchini Sudan amejiuzulu leo siku moja baada ya Jenerali Awad Ibn Auf kutangaza kuwachia wadhifa wa kiongozi wa mpito kutokana na shinikizo la waandamanaji. Salah Abdallah Mohamed Saleh ambaye alikuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa wakati wa utawala wa rais Bashir amekuwa akituhumiwa kufanya mauaji ya waandamanaji wanaotaka kukomesha utawala wa jeshi kwenye kipindi cha mpito. Shirika la habari la taifa SUNA limeripoti kuwa kiongozi mpya wa mpito Jenerali Abdel Fattah al-Burhan ameridhia kujiuzulu kwa bwana Salah.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili ya DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.