Star Tv

Maalfu ya watu wameshiriki katika maandamano makubwa kabisa, kuwahi kufanyika hadi sasa nchini Sudan ya kumtaka Rais wa nchi hiyo Omar al-Bashir ang’atuke baada ya kutawala kwa muda wa takriban miaka 30.

Waandamanaji walikwenda hadi kwenye makao makuu ya jeshi mjini Khartoum, huku wakipaza sauti zao wakisema, amani, haki na uhuru. Makaazi ya rais al-Bashir pia yamo kwenye makao makuu hayo. Waandaaji wamesema kabla ya maandamano hayo kuanza idadi kubwa ya polisi waliwekwa katika sehemu mbalimbali za mji mkuu, Khartoum ambapo waliwazuia wapita njia kuzifikia sehemu kadhaa za mji huo. Kwa mujibu wa taarifa maandamano hayo yalifanyika kwa usalama. Tangu kuanza harakati za wananchi, mnamo mwezi Desemba za kumtaka rais al-Bashir aachie ngazi, watu 31 wameshauawa. Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watche limesema linaamini kwamba watu 51 waliuawa wakiwemo watoto na wahudumu wa afya.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.