Star Tv

Serikali ya Msumbiji imesema visa vilivyothibitishwa vya maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu katika mji wa Beira vimeongezeka maradufu na kufikia wagonjwa 271 katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.

Serikali na wafanyakazi wa mashirika ya kutoa misaada wanajaribu kudhibiti kusambaa kwa maradhi hayo wiki mbili tangu kimbunga Idai kilipoupiga mji wa Beira na kusababisha mafuriko makubwa yaliyowauwa zaidi ya watu 700 katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe na Malawi.

Akizungumza wakati wa kufungua kituo cha muda cha matibabu ya kipindupindu mjini Beira, waziri wa Mazingira wa Msumbiji amesema tayari wagonjwa 138 wanapatiwa matibabu na kwamba hadi sasa hakuna aliyefariki dunia kutokana na maradhi hayo kwenye hospitali zinazotoa huduma.

Maeneo mengi nchini Msumbiji na Zimbabwe ambayo yalipigwa vibaya na kimbunga Idai bado hayafikiki kwa njia ya Barabara. Maradhi ya kipindupindu ni tatizo sugu nchini Msumbiji ambayo imeshuhudia miripuko ya mara kwa mara katika miaka mitano iliyopita na kulingana na shirika la Afya duniani kiasi watu 2000 walipatwa na kipindupindu wakati mlipuko wa mwaka 2018.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.