Star Tv

Idadi ya vifo vilivyosababishwa na mafuriko yalioambatana na kimbunga Idai imeongezeka na kufikia watu 217 huku takriban watu 15,000 wakihitaji huduma za uokozi.

 Waziri wa ardhi na mazingira wa Msumbiji Celso Correia amesema hii leo kwamba watu 3,000 tayari wamekwishaokolewa. Wafanyakazi wa kutoa misaada walipambana kuwasaidia manusura lakini pia kuwafikishia misaada ya kiutu nchini Zimbabwe, Malawi na Msumbiji ambazo zimeathiriwa pakubwa na kimbunga hicho. Baadhi ya vyombo vya habari vinaripoti kwamba zaidi ya watu 300 wamefariki kutokana na janga hilo ikiwa ni siku tano baada ya kimbunga hicho Idai kupiga eneo kubwa la Zimbabwe na Malawi. Kimbunga Idai kilianza kwa kuupiga mji wa bandari wa Beira nchini Msumbiji Alhamisi iliyopita na kisha kuelekea nchini Zimbabwe na Malawi na kusababisha uharibifu mkubwa wa majengo na kuyaweka hatarini maisha ya maelfu ya wakazi.

 

Chanzo: kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.