Star Tv

Zaidi ya watu 86 wameuawa Katikati mwa nchi ya Nigeria katika muendelezo wa mgogoro kati ya wafugaji na wakulima.

Kwa mujibu wa maafisa wa mji huo, mapigano hayo yalianza siku ya Alhamisi baada ya kundi moja la wakulima kutekwa na watano kati yao kuuawa, kabla ya tukio kubwa linalotajwa kuwa la kulipiza kisasi siku ya Jumamosi dhidi ya wakulima.

Mapigano makali yametokea katika vijiji mbalimbali katikati mwa nchi ya Nigeria ndani ya siku chache, yameacha makovu kwa kusababisha vifo vya watu wengi na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Katika eneo la Barkin Ladi mapigano hayo yameshamiri zaidi kiwa ndio eneo ambalo mgogoro umekuwa ukitokea mara kwa mara licha ya kwamba hali ilikua shwari ndani ya miaka miwili iliyopita.

Mapigano yaliripotiwa kutokea tena mwezi April, lakini haya ya sasa yamekithiri.

Tokea kuanza kwa mwaka huu, mapigano haya yaliripotiwa kutokea katika baadhi ya maeneo ya katikati mwa Nigeria, licha ya kutajwa kuwa yalizuiliwa na vikosi vya usalama.

Mapigano haya ambayo ni ya kulipizana visasi, licha ya kusababisha vifo vingi sambamba na majeruhi, pia vimesababisha mgawanyiko mkubwa wa ukabila na udini katika eneo hilo.

Polisi nchini Nigeria tiyari imetuma vikosi vyake katika maeneo yaliyoathirika ili kudhibiti hali ya mambo.

Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.