Star Tv

Msichana raia wa Sudan Noura Hussein ambaye alihukumiwa kifo kwa kumuua mume wake kutokana ya madai kuwa alimbaka amekata rufaa.

"Leo tulikata rufaa kwenye mahakama ya rufaa kupinga uamuzi uliotolewa na mahakama ya chini," wakili wake Al-Fateh Hussein aliliambia shirika la AFP Alhamsi.

Mahakama ya Sudan ilimpata na hatia Bi Hussein kwa kuua makusudi mapema mwezi Mei baada ya familia ya mumewe kukataa kufidiwa fedha.

Hatma ya Bi Hussein ambaye sasa yuko miaka 19, ilizua maoani kote duniani na hata kuanzisha kampeni #HakikwaNoura.

Baba yake Bi Hussein alimalazimisha kuolewa akiwa na miaka 16 na alikua amejaribu kukimbia.Baada ya ya familia kumkabidhi kwa mume wake, Bi Hussein alisema mume wake aliwaita binamu zake waliomshika huku akimbaka.

Alimdunga kisu na kumua mumewe wakati alijaribu tena kumbaka siku iliyofuati.

Mahaka ya sharia ilimhumu kifo kwa kunyongwa.

Wakati huo huo kundi la wanaharakati wa kupigania haki za kibinaadamu la Equality Now limesema kuwa litamwandikia rais Omar al-Bashir kumuomba amuonee huruma.

Shirika la Amnesty International limesema kuwa hukumu ya mwanamke ya kifo ambaye alikuwa akijitetea inaangazia uzembe wa serikali kukabiliana na ndoa za watoto , ndoa za lazima na ubakaji katika ndoa.

Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.