Star Tv

Mahakama ya serikali iliyojitenga ya Somaliland imemfunga jela miaka mitatu ,msichana anayeimba mashairi kwa kosa la kuhamasisha Somaliland kuungana na Somalia .

Makundi ya wanaharakati nchini Somaliland wamesema Bi. Nacima Qorane ameminywa haki zake za kibinadamu.

Somaliland ilijitambulisha kuwa huru mwaka 1991 licha ya kuwa taifa hilo halitambuliwi kimataifa.

Bi.Qorane alikamatwa mwezi Januari baada ya kurejea kutoka Mogadishu,mji mkuu wa Somalia ,wakati ambapo mshtakiwa alisema ametoka kuimba shairi la kuhamasisha umoja wa Somalia.

Baada ya mapigano ya mara kwa mara kaskazini magharibi mwa Somalia,hali hiyo ilisababisha mgawanyiko wa nchi hiyo na hatimaye Somaliland ikajitangaza kuwa iko huru .

Eneo hilo la Somaliland lina wakazi wapatao milioni 3.5 Mwendesha mashtaka amesema msichana huyo amepatikana na makosa ya kuitukana nchi yake na kutokuwa mzalendo wa serikali yake ya Somaliland.

Kituo cha haki za binadamu nchini Somaliland ameiomba serikali ya Somaliland kumuachia huru Nacima Qorane na kuheshimu haki za binadamu.

"Uhuru wa kujieleza ni jambo ambalo linalindwa na katiba ya Somaliland.Hivyo tumeitaka Somaliland kuheshimu katika yake yenyewe."

Mkurugenzi wa kituo hicho Guleid Ahmed Jama aliiambia BBC juu ya hofu yao kwa kukamatwa na kufungwa kwa msichana yule.

Aidha yeye sio wa kwanza kukutana na mashtaka ya namna hii kwa kuwa kuna idadi kubwa ya waandishi wa habari na wasanii waliowahi kufungwa Somaliland kwa kosa la namna hiyo hiyo.

kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.