Star Tv

Watu zaidi ya 37 wamefariki baada ya mafuriko na maporomoko ya ardhi kuukumba mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kinshasa kufuatia mvua kubwa.

Wengi wa waliouawa ni wakazi wa mitaa ya mabanda ambapo nyumba nyingi zimeharibiwa na maji ya mafuriko na maporomo ya ardhi. Wengi kati ya wakazi milioni kumi wa mji wa Kinshasa huishi katika makazi duni katika maeneo tambarare na miundo mbinu ya kuondoa maji taka ni duni.

Waziri wa jimbo anayeangazia masuala ya kiafya na kijamii Dominique Weloli, alisema wengi wa waliofariki ambao ni pamoja na "watoto wawili au watatu waliokufa maji" walikuwa wanaishi Ngaliema, mtaa duni ambao umeathirika sana.

Kumekuwa na matukio ya vifo vinavyotokana na mafuriko karibu kila mwaka msimu wa mvua kubwa.

Kwa hisani ya BBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.