Star Tv

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhesimiwa Dk.Hussein Ali Mwinyi, awasili jijini Luanda Angola.

Mhesimiwa Dk.Hussein Ali Mwinyi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Sherehe za kumuapisha Rais wa Jamhuri ya Angola Mhe. Joao Manuel Goncalves Lourenco, pamoja na Makamu wa Rais Esperanca Maria Eduardo Franscisco da Costa. Sherehe hizo zinatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Afrika na Nje ya Afrika. Katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Angola Quatro de Fevereiro Mheshimiwa Rais Dk. Mwinyi akiambatana na mkewe Mariam Mwinyi na ujumbe alifuatana nao alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Tete Antonia.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.