Star Tv

Waandamanaji katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameshambulia na kuharibu kambi ya vikosi vya Umoja wa Mataifa kushinika ziondoke nchini humo.

Monusco inalaumiwa kwa kushindwa kuleta amani mashariki mwa DRC kwa zaidi ya miaka 20 tangu vikosi hivyo kupelekwa katika eneo hilo linalokumbwa na ghasia.

Picha zilizoshirikishwa katika mitandao ya kijamii zinaonyesha watu wakiimba kupinga uwepo wa vikosi vya kulinda amani nchini DRC, wengine wakiondoa nyenzo za msingi wa kituo chao kikuu huko Goma.

Masoko na maduka mengi yamefungwa Jumatatu katika mji unaokaribia watu milioni moja kwa hofu ya kuzuiwa na waandamanaji, Eliezer Makambo mfanyabiashara wa ndani aliiambia BBC Maziwa Makuu.

Msemaji wa serikali, Patrick Muyaya, amesema kwenye Twitter kwamba serikali "inalaani aina yoyote ya mashambulizi dhidi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na majengo".

Muyaya ameongeza kwa kubainisha waliohusika na maandamano ya Jumatatu mjini Goma "wataadhibiwa vikali".

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.