Star Tv

Mkuu wa Umoja wa Afrika, Rais Macky Sall wa Senegal, ameeleza "wasiwasi mkubwa" kutokana na kuongezeka kwa mvutano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda.

Rais Sall amebainisha kwamba kila nchi inaishutumu nyingine kwa kuunga mkono makundi ya waasi yenye silaha ambapo ameomba kuwepo na utulivu na kuzitaka pande zote mbili kutatua mzozo wao kupitia mazungumzo.

Siku ya Jumamosi Rwanda ilisema wanajeshi wake wawili Élysée Nkundabagenzi na Ntwari Gad walikuwa wakishikiliwa mateka mashariki mwa DR Congo na wanamgambo wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR, ambayo inasema inapata uungwaji mkono kutoka Kinshasa.

Hapo awali, DR Congo ilisitisha safari za ndege kuelekea Rwanda na kumwita balozi wa Kigali ikimtuhumu jirani yake kuwaunga mkono waasi wa M23, ambao sasa inawataja rasmi kuwa magaidi.

Kundi la M23 pia limetengwa katika mazungumzo ya amani ya Nairobi kati ya serikali ya Congo na makundi mengi ya wanamgambo wanaopigana katika eneo lake la mashariki.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.