Senegal imemzawadia kila mchezaji wa timu ya taifa ya kandanda zawadi ya pesa taslimu na mashamba kufuatia ushindi wao katika Kombe la Mataifa ya Afrika.
Kila mchezaji wa timu alipokea zaidi ya $87,000 (£64,000) na kiwanja katika mji mkuu, Dakar, na katika mji jirani wa Diamniadio wakati wa sherehe iliyofanyika ikulu ya rais.
Rais Macky Sall pia aliteua timu hiyo katika Tuzo ya heshima kutoka kwa Rais ambayo ni maarufu nchini Senegal, huku mashabiki wakishangilia nje ya lango.
Rais hapo awali aliishukuru timu hiyo kwa kufika “kilele cha dimba hilo la Afrika” na kuleta ”fahari na heshima ambayo inaashiria watu wa kipekee. ”
Senegal iliishinda Misri kwa mikwaju ya penalti 4-2, na kuwa mabingwa wa michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yao.
#ChanzoBBC