Star Tv

Kundi la vijana nchini Nigeria, chini ya mwamvuli wa Bunge la Vijana wa Kaskazini, limetoa wito kwa mfanyabishara tajiri zaidi Afrika Aliko Dangote, viongozi wengine wa wafanyabiashara na wataalamu kuingilia kati uchaguzi wa rais wa 2023.

Vijana hao wanasema kuwa uzoefu wao itasaidia kuleta maendeleo Nigeria.Katika taarifa kundi hilo ambalo lilifadhiliwa na Katibu Mkuu wake Desmond Minakaro na Baraza la Wawakilishi, Mohammed Salihu Danlami alisema watu kama Dangote, Femi Otedola, Mike Adenuga, Akinwumi Adesina, Herbert Wigwe, Ngozi Okonjo Iweala na kadhalika wana uwezo wa kuchukua nafasi ya rais wa Nigeria.

Vijana hao wametoa ushawishi wao kwamba “wafanyabiashara wanaojua jinsi ya kupata faida sasa wanapaswa kuitawala Nigeria”.

Hata hivyo seneta Shehu Sani amesema haoni haja ya Bw. Dangote kuingilia siasa na kwamba anamtaka aendelee kuwa maarufu kutokana na utajiri wake mbali na siasa.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.