Star Tv

Polisi nchini Somalia wamethibitisha vifo vya raia katika bomu lililotegwa ndani ya gari katika mji mkuu Mogadishu, televisheni ya taifa imeripoti.

Watu takriban 17 wamejeruhiwa, wakiwemo watoto 13 kutoka shule jirani na eneo la tukio.

Mlipuaji mabomu wa kujitoa mhanga wa kikundi cha al-Shabab aliyekuwa anaendesha gari lililosheheni vilipuzi alilenga msafara wa kampuni ya usalama ya kibinafsi, Duguf, ambayo ilipewa kandarasi ya kulinda Umoja wa mataifa.

Polisi haikusema iwapo wafanyakazi wa Umoja wa mataifa waliumia katika shambulio hilo.

Vyombo vya habari nchini humo vimesema kuwa mlipuko huo ulitokea wakati wa msongamano wa magari karibu na makutano yanayofahamika kama 'Kilometre Four Junction'.

Kundi lenye uhusiano na Al-Qaeda la wanamgambo wa al-Shabab limethibitisha kutekeleza shambulio hilo.

Vyanzo vya habari vinavyounga mkono al-Shabab media vimesema wanamgambo hao waliwalenga “maafisa wa kijeshi wazungu”.

Mara kwa mara Al-Shabab wamekuwa wakiwalenga maafisa wa vikosi vya usalama na serikali mjini Mogadishu.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.