Star Tv

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera amewafuta kazi Waziri wa Nishati na mkuu wake wa watumishi ambao wanakabiliwa na mashtaka ya ufisadi.

Wawili hao na afisa mwingine mmoja Enock Chihana, mshirika katika usimamizi wa Tonse Alliance walikamatwa siku ya Jumatatu kwa madai ya kuhusika na zabuni ya mafuta ya nchi hiyo.

Watumishi wa serikali katika wizara nyeti waliripotiwa kujaribu kushawishi jinsi kandarasi ya usambazaji wa mafuta itakavyotolewa.

Nafasi ya waziri Newton Kambala haijajazwa baada ya kufutwa kwake, Ambapo kwasasa majukumu ya wizara ya nishati yamehamishiwa ofisi ya rais.

Mrithi wa mkuu wa watumishi wa umma Chris Chaima Banda pia hajatajwa wakati tangazo la kufutwa kwake lilipotolewa.

Aidha, Bw. Kambala na Bw. Banda hawajatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.