Star Tv

Mfalme Goodwill Zwelithini wa jamii ya Wazulu nchini Afrika Kusini amefariki dunia hospitalini ambako alikuwa anapokea matibabu ya ugonjwa wa kisukari.

Mfalme huyo aliyekuwa na umri wa miaka 72, alikuwa kiongozi wa kabila kubwa zaidi Afrka Kusini na kiongozi mashuhuri wa kitamaduni.

Mfalme huyo alikuwa amelazwa katika hospitali ya Kwa Zulu-Natal wiki iliyopita kufuatilia hali ya kisukari iliyokuwa inamsumbua.

 Waziri mkuu wa mfalme huyo ameishukuru Afrika Kusini kwa kuendelea kumuombea na kutoa msaada katika kipindi hiki kigumu.

 Mflame Goodwill Zwelithini aliongoza jamii ya Wazulu chini ya kifungu cha sheria ya utawala wa kitamaduni katika Katiba ya Afrika Kusini tangu alipofariki baba yake mwaka 1968.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.