Star Tv

Serikali ya Ethiopia imeishutumu Sudan kuchochea mgogoro kati ya mataifa mawili ambayo yamekuwa katika mvutano kutokana na mzozo wa mpaka.

Ghasia ziliibuka mwishoni mwa mwaka jana kuhusu eneo la wakulima wa Ethiopia ambao Sudan wanasema waliingia katika eneo lao.

Pande zote mbili zimekuwa zikishutumiana kwa kusababisha ghasia.

Mvutano umekuja wakati Ethiopia ikiwa na mgogoro kaskazini mwa ukanda wa Tigray.

Katika taarifa kali iliyotolewa na serikali ya Ethiopia, imelishutumu jeshi la Sudan kuchochea mvutano huo kuingia kwenye vita.

Licha ya kudai mzozo huu kuhusiana mvutano wa eneo la wafugaji walioko karibu na mpaka lakini inaonekana wazi masuala ya kisiasa kuhusika pia.

Taarifa ya Ethiopia imesema jeshi la Sudan linachochea mgogoro ili kuinufaisha Misri.

Kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya Ethiopia na serikali ya Misri juu ya ujenzi wa bwawa katika mto Nile.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.