Star Tv

Mahakama ya kijeshi ya Uganda imewahukumu kifungo cha siku 90 jela wanajeshi 7 baada ya kushtakiwa kwa kuwashambulia waandishi wa habari.

Jeshi la Uganda UPDF katika taarifa yake limesema kamati ya nidhamu ya jeshi imewahukumu wanajeshi hao akiwemo afisa wa cheo cha Kapteni, pamoja na kuwapa onyo kali.

Matukio ya kushambuliwa waandishi yameongezeka katika miezi ya hivi karibuni nchini Uganda, hasa wakati ambapo kumekuwa na operesheni za kuwakamata wafuasi wa kiongozi wa upinzani Bobi Wine.

Mnamo siku ya Jumatano wanajeshi walilivamia kundi la waandishi wa habari nje ya ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ambapo waliwapiga na 20 miongoni mwao walijeruhiwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.