Star Tv

Polisi wamemkamata mwanamume mmoja aliyejulikana kwa jina la Abubakar Amodu mwenye umri wa miaka 20, ambaye alipanga njama na genge moja na kumteka nyara baba yake mzazi na baadaye akapokea milioni 2 za Nigeria kama fidia.

Amodu ni miongoni mwa watu 25 waliokamatwa na afisa wa ofisi ya uhusiano mwema katika polisi ya Nigeria, CP Frank Mba, kwa makosa kadhaa waliotekeleza mjini Abuja.

Kijana huyo aliyekamatwa pamoja na wahalifu wengine, alifaya kazi na baba yake ambaye ni mfugaji.

Kijana huyo aliwaambia wanahabari kuwa baba yake alikuwa anafuga ngombe na kwamba alipewa ngombe 15 na akaamua kuondoka nyumbani.

Alitoa ushahidi vile alivyoanza urafiki na genge hilo la wahalifu waliomshauri kumteka nyara baba yake kwasababu hiyo ilikuwa njia pekee ya kumuwezesha kutengeneza pesa kwa njia rahisi na kutajirika kwa haraka.

Kijana huyo anakiri kwamba, binafsi alipokea milioni mbili pesa taslim za Nigeria kama fidia iliyotumwa ili baba yake aachiwe huru.

Chanzo na BBC Swahili.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.