Star Tv

Mapigano yametokea kati ya kundi la wanamgambo wa Maï-Maï na vikosi vya jeshi la serikali, FARDC, katikati mwa mji mkuu wa Katanga, ya zamani Kusini Mashariki mwa DRC.

Mapigano hayo yametokea usiku wa Ijumaa kuamkia leo Septemba 26,2020, Ambapo milio ya risasi na milipuko imeendelea kusikika mapema leo Jumamosi aljafajiri karibu na Chuo Kikuu.

Wanamgambo hao waliingia katika mji wa Lubumbashi usiku wakipitia maeneo kadhaa ya mji huo.

Vyanzo vya polisi kupitia Waziri wa Mambo ya Nje Philibert Kunda Milundu amesema wamethibitisha tukio hilo katika mkoa huo na vinahakikisha kuwa wapiganaji hao ni kutoka kundi la wanamgambo la Bakata Katanga, lililojitenga kutoka kundi la Maï-Maï.

Waziri Milundu amesema wanajeshi wamegizwa kutowapiga risasi wanamgambo hao, Huku hali ya wasiwasi pia inaripotiwa katika mji wa Likasi.

Mapigano hayo yanatokea baada ya jaribio la wafungwa kutoroka kutibuliwa siku ya Ijumaa katika gereza la Kasapa huko Lubumbashi.

Chanzo: rfi Swahili.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.