Mapigano yametokea kati ya kundi la wanamgambo wa Maï-Maï na vikosi vya jeshi la serikali, FARDC, katikati mwa mji mkuu wa Katanga, ya zamani Kusini Mashariki mwa DRC.
Mapigano hayo yametokea usiku wa Ijumaa kuamkia leo Septemba 26,2020, Ambapo milio ya risasi na milipuko imeendelea kusikika mapema leo Jumamosi aljafajiri karibu na Chuo Kikuu.
Wanamgambo hao waliingia katika mji wa Lubumbashi usiku wakipitia maeneo kadhaa ya mji huo.
Vyanzo vya polisi kupitia Waziri wa Mambo ya Nje Philibert Kunda Milundu amesema wamethibitisha tukio hilo katika mkoa huo na vinahakikisha kuwa wapiganaji hao ni kutoka kundi la wanamgambo la Bakata Katanga, lililojitenga kutoka kundi la Maï-Maï.
Waziri Milundu amesema wanajeshi wamegizwa kutowapiga risasi wanamgambo hao, Huku hali ya wasiwasi pia inaripotiwa katika mji wa Likasi.
Mapigano hayo yanatokea baada ya jaribio la wafungwa kutoroka kutibuliwa siku ya Ijumaa katika gereza la Kasapa huko Lubumbashi.
Chanzo: rfi Swahili.