Wizara ya Afya ya Uganda imesema kuwa idadi ya wagonjwa wa corona nchini humo imefikia 101 kutoka wagonjwa 100.
Idadi hiyo imepanda baada ya Mtanzania mmoja ambaye ni Dereva wa Lori kutoka nchini Tanzania mwenye umri wa miaka 32 kubainika kuwa na corona baada ya kupimwa.
Wizara hiyo imesema Dereva huyo aliingia Uganda kupitia mpaka wa Mtukula akitokea Tanzania.
Pia imetoa taarifa ya wagonjwa waliopona corona nchini humo kuwa ni 55 na imesema hakuna kifo kitokanacho na ugonjwa huo mpaka sasa.