Star Tv

Serikali ya Kenya imetangaza kuwa itaanza kufungua hoteli zake kwa kuzingatia masharti ya kuwapima wahudumu wa afya na ikiwa hawatakuwa na maambukizi ya virusi vya Corona ndio wataweza kuhudumu kwenye hoteli hizo.

Taarifa hii ya hoteli kuanza kufunguliwa imetangazwa na Waziri wa Afya nchini humo Mutahi Kagwe ambapo amesema kuwa hoteli hizo zitahitajika kufuata kanuni zitakazowekwa kama vile kuhakikisha kuwa hakuna misongamano katika hoteli hizo.

Idadi ya watu waliopona virusi vya Corona imetajwa kuongozeka nchini humo na kufikia 114 baada ya watu 8 hii leo kuruhusiwa kutoka hospitalini.

Aidha, Waziri Kagwe amesema pia wagonjwa wameongezeka na kufikia 363 kwa ongezeko la watu 8  waliokutwa na maambukizi kuongezeka leo baada ya kupimwa na kukutwa na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Wagonjwa hao 8 walioripotiwa leo wote wametolewa ufafanuzi kuwa ni raia wa Kenya na wala hakuna wa nje ya nchi hiyo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.