Star Tv

Rais Uhuru Kenyatta amepinga kufanyika kwa mazungumzo yoyote na kiongozi wa upinzani Raila Odinga kumaliza mgogoro wa kisiasa nchini Kenya uliosababishwa na uchaguzi mkuu uliokwisha.

Katika hotuba yake muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa marudio , Rais Kenyatta amesema kuwa mpinzani wake mkuu Raila Odinga atakwenda mahakamani kwa mara nyengine tena kupinga uchaguzi wake.

Kenyatta amewataka wapinzani wake wa Nasa kutumia njia zote za kisheria katika kupigania haki yao.

Wawacheni mwanzo watumie njia zote za kisheria zilizosalia wawacheni wafanye wanachotaka.

Hakuna mtu yeyote atakayewadhulumu haki yao ya kikatiba.

''Kuhusu ajenda yangu ya kusonga mbele nitazungumza baada ya makabiliano ya mahakamani yamekwisha'' , alisema Kenyatta katika makao makuu ya tume ya uchaguzi katika eneo la Bomas jijini Nairobi.

Rais Kenyatta pia alimshutumu Raila Odinga kwa kujiondoa katika uchaguzi huo.

''Licha ya kwamba mpinzani wangu mkuu alienda mahakamani akitaka uchaguzi wa urais kufutiliwa mbali na akakubaliwa, aliamua kutotilia maanani uamuzi wote kwa pamoja ambao uliagiza kufanyika kwa uchaguzi katika kipindi cha siku 60 uliosimamiwa na IEBC.Baadaye alikaataa kushiriki katika uchaguzi''.

Katika uchaguzi wa marudio Uhuru alijipatia kura 7,483,895 huku Raila Odinga akijipatia kura 73,228 hata baada ya kujiondoa katika uchaguzi huo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.