Star Tv

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, limepitisha azimio la kutaka kupitishwa kwa sheria ya kupiga marufuku utengenezaji na uingizwaji wa sabuni na vipodozi vyenye viambata vya sumu
vinavyodaiwa kuathiri afya za watumiaji hususani wanawake.

Hoja kuhusu katazo hilo imewasilishwa bungeni na Gideon Thoar, mbunge kutoka Sudan kusini, ambaye kwa kuzingatia vifungu kadhaa vya mkataba wa uanzishwaji wa jumuia ya Afrika Mashariki, kuhusu usalama wa bidhaa na kulinda afya ya mlaji, alitaka baraza la Mawaziri la jumuiya hiyo kukubali hoja na azimio la kupiga marufuku
uzalishaji, uingizwaji na matumizi ya sabuni na vipodozi vyenye Hydroquinone katika nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki.

Pamoja na kelele zinazopigwa na wana sayansi na magwiji wa tiba, vipodozi vyenye viambata vya sumu vinadaiwa kuendelea kuingizwa kwa wingi na kutumiwa katika nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki. Mbunge Oda Gasinzigwa kutoka Rwanda, anasema hii ni ishara kuwa watumiaji wameukataa U-afrika wao.

Baadhi ya wabunge kutoka Burundi na Tanzania hususani wanawake, wanasema marufuku ya uingizaji na utumiaji wa vipodozi hivyo, itafanikiwa iwapo itakwenda sambamba na utoaji wa elimu kwa wananchi. Baada ya kupitishwa na bunge, hatua itakayofuata na kuwasilishwa kwenye mamlaka husika kwa hatua za kisheria.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.