Wanawake wanaoishi vijijini huko Jamhumuri ya Kidemokrasi ya Kongo, hawana haki ya urithi wa mali pamoja na ardhi iliyoachwa na wazazi wao au waume zao. Na hii inatokana na mila na desturi zao zinazomtambua mwanaume kama mrithi pekee wa Ardhi.
Wanaharakati wa haki za wanawake nchini humo wako katika jitihada za kuwaelimisha jamii kuhusiana na madhara ya mila hizo. Wanaweke wanaoishi vijijini katika jimbo la Congo central hawana haki ya urithi mali au ardhi ya wazazi au waume zao.
Mila ya jimbo hilo inapinga kabisa kumpa mke urathi. Alphonsine Ponga ni mwanaharakati wa kutetea haki za akina mama katika kijiji cha Mbaza Ngungu. Yeye pia alikuwa mwathirika wa utamaduni huu.
Ponga ameeleza kwamba sheria ya Congo haina ubaguzi katika suala la urithi. Lakini katika hali kawaida , ni mila ndo imeendelea kukithiri zaidi ya sharia ya nchi hasa katika maeneo ya vijijini.