Star Tv

Marudio ya kura za urais nchini Kenya yanaendelea. Katika maeneo mengi Kisumu, mji ambao ni ngome ya Raila Odinga, wakazi wamefunga barabara na kuchoma matairi wakipinga marudio ya kura za urais. Kinara wa upinzani NASA alikuwa amewahimiza wafuasi wake kutoshiriki kwenye kura za leo.

Polisi nchini humo wasema raia mmoja aliyepigwa risasi na polisi katika maandamano yenye vurugu amefariki dunia akiwa hospitali. Tukio hilo limetokea Kisumu na imeripotiwa kuwa vijana wengine watu waejeruhiwa na risai na wapo hospitalini.

Licha ya haya, kura zimeendelea kwenye maeneo mengine ila idadi ya wapiga kura imekuwa ndogo sana ikilinganishwa na uchaguzi uliopita. Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee amepiga kura yake katika eneo la Mutomo, Gatundu katika kaundi ya Kiambu.

Amesema amefurahia kwamba raia wanajitokeza kupiga kura. "Tumechoshwa na uchaguzi na sasa ni wakati wa kusonga mbele. Uchaguzi ni fursa kwa raia kuwachagua viongozi kama ilivyosema Mahakama ya Juu. Hebu tuwachague viongozi na tusonge mbele," amesema.

Kwa Hisani ya BBC Swahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.