Star Tv

Waziri wa elimu nchini Kenya George Magoha amewakumbusha walimu kwamba adhabu ya viboko imesalia kuwa marufuku katika shule za nchini humo.

Akiwa ziarani katika eneo la Pwani Magoha amesema walimu watakaopatikana wakiwapiga wanafunzi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Kauli yake inajiri siku chache baada ya mwanafunzi katika eneo hilo kupigwa kwasababu ya kula chapati tano ikiwa ni zaidi ya zile ambazo walikuwa wamepangiwa kula.

Kipigo hicho kilimfanya mwanafunzi huyo wa kiume kupata majeraha kwenye figo na sehemu zake za siri na kulazwa hospitalini.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo na mwalimu mwingine walikamatwa na maafisa elimu mkoani humo walifunga shule hiyo baada ya ukaguzi kuonesha haijasajiliwa na ina masuala ya usafi.

Waziri Magoha amesema shule ambazo zina masuala ya kufuata sheria zitafungwa na wanafunzi kuchukuliwa katika shule za jirani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.