Star Tv

Wasafiri kutoka Dubai wataruhusiwa kuingia nchini Kenya kuanzia leo baada ya nchi hiyo kuondoa marufuku iliyokuwa imeweka kwa ndege zote zinazoingia na za abiria kutoka taifa hilo la Mashariki ya Kati wiki mbili zilizopita.

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kenya (KCAA) Gilbert Kibe ameliambia gazeti la Business Daily kwamba marufuku hiyo iliondolewa Jumatatu usiku wa manane, na kutoa afueni kubwa kwa mamia ya wasafiri kati ya maeneo hayo mawili.

Kenya ilikuwa imesimamisha safari zote za ndege za abiria zinazoingia na kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) mnamo Januari 10 kulipiza kisasi dhidi ya hatua ya Dubai kupiga marufuku safari zote za ndege za abiria kutoka Kenya kwa madai ya vipimo bandia vya Covid-19.

Marufuku hiyo hata hivyo haikuathiri safari za ndege za mizigo ambazo kwa kawaida husafirishwa na wachukuzi kama vile Kenya Airways (KQ) na shirika la ndege la Emirates kutoka UEA hadi Kenya.

"Kenya itafanya NOTAM kuondoa kusimamishwa kwa safari za ndege kwenda na kutoka UAE kuanzia usiku wa manane leo (Jumatatu)''-alisema Bw Kibe.

Marufuku hiyo ilikuja siku chache baada ya UAE kuongeza muda wa marufuku ya safari za ndege nchini Kenya baada ya kubaini kuwa wasafiri kutoka Nairobi walipimwa na kukutwa na Covid-19 baada ya kuwasili katika taifa hilo la Mashariki ya Kati, licha ya nyaraka zao kuonesha hawana maambukizi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.