Star Tv

Maafisa wa Kenya wamethibitisha mlipuko wa homa ya virusi vya mafua aina ya Influenza nchini humo.

Taasisi ya utafiti wa tiba nchini Kenya (Kemri) ilisema kuwa sampuli kati ya 36 zilipatikana na homa ya influenza A.

Hospitali ya kitifa ya Kenya -Kenyatta National Hospital (KNH) inatoa chanjo ya mafua ya mlipuko wa mafua (aina ya Influenza A)

KNH imesema kwa sasa inatoa chanjo hiyo kwa wahudumu afya tu, katika juhudi zinazoungwa mkono na chuo kikuu cha kitaifa cha Washington, ambacho kinafanya utafiti wa magonjwa nchini Kenya.

“Anayefika wa kwanza ndiye anayepokea chanjo hiyo na watu 400 wanaweza kuchanjwa kila siku,” KNH imesema.

Hii inakuja wakati Taasisi ya tiba ya Kenya iliyopo mjini Kisumu ilisema ufuatiliaji baina ya Septemba na Novemba mwaka huu kuonyesha kuwa kulikuwa na mlipuko wa Infuenza A.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.