Maafisa wa Kenya wamethibitisha mlipuko wa homa ya virusi vya mafua aina ya Influenza nchini humo.
Taasisi ya utafiti wa tiba nchini Kenya (Kemri) ilisema kuwa sampuli kati ya 36 zilipatikana na homa ya influenza A.
Hospitali ya kitifa ya Kenya -Kenyatta National Hospital (KNH) inatoa chanjo ya mafua ya mlipuko wa mafua (aina ya Influenza A)
KNH imesema kwa sasa inatoa chanjo hiyo kwa wahudumu afya tu, katika juhudi zinazoungwa mkono na chuo kikuu cha kitaifa cha Washington, ambacho kinafanya utafiti wa magonjwa nchini Kenya.
“Anayefika wa kwanza ndiye anayepokea chanjo hiyo na watu 400 wanaweza kuchanjwa kila siku,” KNH imesema.
Hii inakuja wakati Taasisi ya tiba ya Kenya iliyopo mjini Kisumu ilisema ufuatiliaji baina ya Septemba na Novemba mwaka huu kuonyesha kuwa kulikuwa na mlipuko wa Infuenza A.
#ChanzoBBC