Star Tv

Bodi ya Filamu Kenya inasema kuwa filamu kuhusu maisha ya wanandoa wa jinsia nchini Kenya imepigwa marufuku nchini humo.

Katika taarifa KFCB imesema filamu ya I am Samuel, inahamasisha ndoa ya wapenzi wa jinsia moja ambayo inakiuka sheria inayoharamisha ushoga.

Iliongeza kuwa filamu hiyo pia ilikuwa "inabeza katiba inayotambua familia kama msingi wa jamii na inafafanua ndoa kuwa kati ya watu wawili wa jinsia tofauti".

"Jaribio la kufanya onyesho, kusambaza, kutangaza au kuwa na filamu hiyo iliyopigwa marufuku nchini Kenya kutakabiliwa kisheria,”- Chris Wambua, Kaimu Mkuu wa Bodi ya Filamu, aliwaambia wanahabari.

Filamu hiyo, iliyoelekezwa na Peter Murimi, ilitolewa mwaka jana, ni filamu iliyoandaliwa kwa zaidi ya miaka mitano na inaangazia uhusiano wa Sam na mpenzi wake Alex dhidi ya kuongezeka kwa vurugu na ubaguzi.

Aidha, KFCB ilitoa uamuzi juu ya filamu hiyo kwani ilikuwa imeombwa kuipa uainishaji.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.