Star Tv

Naibu wa Rais nchini Kenya William Ruto amemjibu waziri wa msuala ya ndani nchini Kenya Fred Matiangi kufuatia matamshi yake mbele ya kamati moja ya bunge siku ya Jumatano.

Kulingana na taarifa ilitolewa na msemaji wake David Mugonyi, na kunukuliwa na gazeti la The People Daily nchini Kenya, naibu huyo amemkosoa waziri Matiangi kwa kutoa matamshi yasio na msingi.

Kulingana na naibu huyo lengo la Matiangi katika kikao hicho cha kamati ya bunge lilikuwa kumdhalilisha na kumkejeli yeye na afisi yake.

"Kulingana na matamshi yaliotolewa na waziri Matiangi hakuna ushahidi kwamba anataka kuelewa katiba ama hata wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa naibu wa rais’’-alisema Mugonyi.

Aidha, taarifa yake iliendelea kufafanua kuwa "Bwana Matiangi ametumia vibaya rasilimali ya umma na uwezo wa ofisi yake kwa maslahi ya kisiasa ili kumdhalilisha na kuikejeli ofisi ya William Ruto kwa propaganda za kisiasa’’.

Kulingana na Gazeti la The People, amemshtumu Matiangi na kusema hatua yake inahatarisha usalama wa maisha ya naibu wa rais William Ruto.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.