Star Tv

Kampuni ya ndege ya Rwanda, Rwandair imesitisha kwa muda safari zake katika mataifa ya Afrika Kusini, Zimbabwe na Zambia.

Kampuni hiyo imesema imechukua uamuzi huo kutokana na aina mpya ya Covid-19 inayoripotiwa katika mataifa ya kusini mwa Afrika.

Safari zote za kutoka na kuelekea katika miji ya Johannesburg, Cape Town, Lusaka na Harare zimesitishwa mara moja kuanzia Jumatatu.

Kampuni hiyo ya ndege imewatolea wito wateja wake waombe kurudishiwa fedha na kupanga upya safari zao.

Taarifa kamili ya kuahirishwa kwa safari za Rwandair ilitumwa kwenye mtandao wa kijamii wa twitter.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.