Star Tv

Serikali ya Somalia imekatisha uhusiano wa kidiplomasia na nchi ya Kenya.

Nchi hiyo imewaita nyumbani wanadiplomasia wake wote kutoka Nairobi na kuwapatia wanadiplomasia wa Kenya muda wa siku 7 kuondoka nchini humo.

Tangazo hilo limetolewa na Waziri wa Habari Osman Abukar Dubbe katika chombo cha habari cha kitaifa.

"Serikali ya Somali, kulingana uhuru wake iliyohakikishiwa na sheria ya kimataifa, inatekeleza wajibu kwa mujibu wa katiba ili kulinda utaifa, umoja na ustawi wa nchi imeamua kukatiza uhusiano wake wa kidiplomasia na serikali ya Kenya"- alisema.

Hatua hiyo inakuja baada ya Somalia kuwasilisha barua ya malalamiko dhidi ya Kenya kwa Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Viongozi wa nchi wanachama wa muungano wa maendeleo Afrika Mashariki na pembe ya Afrika (IGAD).

Hivi karibuni Somalia iliituhumu Kenya kwa kuingilia masuala yao ndani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.