Star Tv

Jeshi la Kenya Defence Forces (KDF) limendelea kuwa na umaarufu wake katika Bara la Afrika kutokana na mafunzo na ushirikiano na nchi kama Israel, Marekani na Uingereza.

Hatua hii ya KDF kudhihirika kuwa ni maarufu barani Afrika inakuja wakati jeshi lilipoadhimisha kumbukizi ya siku yake hapo jana Octoba 14, inayojulikana kama KDF Day.

Hata hivyo tishio kubwa linaloendelea kuyakabili majeshi ya ukanda huu ni kundi la kigaidi la Al shabab ambalo limesababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine kulazimika kutoroka jeshini.

Jeshi la Kenya linaendelea kukabiliana na mashambulizi mbalimbali nchini Somalia na Kenya.

Tarehe 14 Oktoba ni siku ya wanajeshi wa Kenya maarufu kama 'KDF day', Ambapo rais Uhuru Kenyatta alihudhuria sherehe hizo katika kambi ya kijeshi ya Lanet huko Nakuru.

Rais Kenyatta alitumia fursa hiyo kuwakumbuka wanajeshi waliofariki dunia katika vita dhidi ya kundi la Al Shabab nchini Somalia, huku Wanajeshi wa Kenya na jamaa zao wakishiriki kwa amani sherehe hizo maalum kuadhimisha siku hiyo ya idara ya jeshi la Kenya KDF.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.