Star Tv
Mazishi ya Malkia Elizabeth II aliyekuwa kiongozi mkuu wa taifa la Uingereza ambaye alifariki Septemba 08, 2022 yatafanyika leo Septemba 19, 2022 jijini London nchini humo.
Mwili wake utasafirishwa kwanza hadi Westminster Abbey kwa ibada ya kidini mbele ya maelfu ya watu, na kisha kuelekea kasri la Windsor kwa ibada ya kifamilia na watu wa karibu zaidi, hatimaye, maziko ya kibinafsi.
 
Wakuu wa nchi kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni wamekuwa wakiwasili kuungana na washiriki wa familia ya Kifalme kukumbuka maisha na huduma ya Malkia.
 
Wanachama wa familia za kifalme kutoka kote Ulaya, ambao wengi wao walikuwa ndugu wa damu wa Malkia wanatarajiwa kushiriki katika mazishi hayo akiwemo Mfalme Philippe wa Ubelgiji na Malkia Mathilde, Mfalme Felipe wa Uhispania na Malkia Letizia.
 
Aidha pia viongozi mbalimbali kutoka Afrika tayari wamewasili akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.