Star Tv

Waziri wa Utamaduni, Sana na Michezo Innocent Bashungwa ameonya tabia ya mashabiki wa timu kubeza timu zao pindi zinaposhindwa kufikia malengo au hatua iliyotamaniwa na mashabiki husika akisema kitendo hicho siyo cha kizalendo na kinawavunja moyo wachezaji.

Waziri Bashungwa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, katika kilele cha mashindano ya mpira wa miguu wa jimbo la Korogwe yaliyopewa jina la Dkt. Kimea Cup

Waziri Bashungwa amesema Watanzania hawana budi kutambua kuwa michezo mingi humalizika kwa matokeo ya aina tatu, ambayo ni kufunga, kufungwa na kutoa sare, hivyo mashabiki hawana budi kuwa tayari kuyapokea matokeo yote matatu.

“Nyinyi nyote mnaoshindana leo ni wazuri ndiyo maana mmefikia fainali, hivyo nyote ni wangu lakini lazima mjue kwamba kwenye mchezo wa mpira wa miguu kuna kushinda, kushindwa na kupata sare, yote ni matokeo na yote lazima watanzania tuwe tayari kuyapokea”- alisema Waziri Bashungwa wakati akizungumza kabla ya mchezo baina ya timu mbili zilizoingia fainali katika mashindano hayo.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Korogwe Mjini Dkt. Alfred Kimea amesema mashindano hayo yameinua vipaji vya vijana wengi katika jimbo la Korogwe mji, ambavyo atahakikisha kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Serikali wanaendeleza vipaji hivyo vya soka kwa manufaa ya vijana na jamii nzima ya Korogwe na Tanga kwa ujumla.

Mashindano ya Dkt. Kimea Cup yalishirikisha timu 12 kutoka kwenye kata 11 za Jimbo la Korogwe mji na kuziwezesha timu ya kata ya Kwamndolwa na kata ya Mgombezi kuingia katika fainali ya mashindano hayo, mchezo uliochezwa katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Korogwe (Korogwe TCC) Novemba 21, 2021.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.