Star Tv

Waendesha mashtaka wa Ufaransa wamefungua uchunguzi kuhusu madai ya ubakaji katika ikulu ya rais mjini Paris.

Vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kwamba mwanajeshi wa kike amesema alinajisiwa baada ya tafrija ya vinywaji katika jumba la Élysée mwezi Julai.

Rais Emmanuel Macron alikuwa amehudhuria hafla hiyo, iliyofanyika kwa wafanyakazi wanaoondoka.

Mtuhumiwa pia mwanajeshi ambaye amehojiwa, lakini bado hajafunguliwa mashtaka rasmi, ripoti zinasema.

Gazeti la Libération liliripoti kwanza mashtaka hayo siku ya Ijumaa.

Wote wawili wanaodaiwa kuwa mwathiriwa na mshambulizi waliripotiwa kufanya kazi katika ofisi ya wafanyakazi wa ulinzi mkali katika jengo hilo, na Libération ilisema wanafahamiana.

Afisa wa rais aliliambia shirika la habari la AFP kwamba "mara tu mamlaka zilipofahamu madai haya, hatua zilichukuliwa mara moja" kumsaidia mwathiriwa huyo.

Aidha mwathiriwa wa tukio hilo na mtuhumiwa wote wamehamishwa katika majukumu mengine, ikulu ilisema.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.