Star Tv

Waziri wa Biashara na uchumi nchini Ufaransa Franck Riester amezindua magari ya umeme yaliyoundwa na kampuni ya E-Motion Africa hapa nchini.

Kampuni ya E-Motion Africa iliundwa mnamo 2019 kwa lengo la kutoa suluhisho la asili na rahisi kwa changamoto ya usafiri unaotoa gesi ya kaboni hapa nchini na inapendekeza kubadilisha injini ya dizeli ya magari ya uchukuzi kuwa magari ya umeme, unayotumia na nguvu ya betri.

Kwa mujibu wa gazeti la The Citizen Waziri Riester amenukuliwa akisema “Gari lisilotoa gesi chafu ndio gari la siku zijazo”.

Riester amesema Ufaransa imejitolea kukuza ushirikiano na kushirikiana kiteknolojia na Tanzania.

Mradi huo ulianzishwa na kampuni ya safari ya Ufaransa Mount Kilimanjaro Safari Club (MKSC) ambayo imekuwa ikifanya kazi kwa miaka 20 Kaskazini mwa nchi katika mbuga za kitaifa.

#ChanzoTheCitizenNaBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.