Star Tv

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amezikwa nyumbani kwake katika kijiji cha Mtambwe Nyali mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mwili wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, uliagwa mapema leo asubuhi katika msikiti wa Maamur Upanga jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa Zanzibar kwa ajili ya mazishi.

Viongozi mbalimbali wa kitaifa walishiriki ibada hiyo akiwemo Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na Kiongozi wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe.

Baadhi ya wananchi pamoja na viongozi waliohudhuria ibada ya mazishi ya Maalim Seif Sharif wamesema kuwa wamesikitishwa sana na msiba wa kiongozi huyo.

Mamia ya wazanzibari walijitokeza katika Viwanja vya Mnazi Mmoja vilivyopo mjini Unguja ambapo ndipo mwili ulipokelewa kutoka jijini Dar es Salaam kwa ajili ya dua kabla ya kusafirishwa kwenda kijijini kwake Mtambwe.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.