Star Tv

Tembo 170 watapigwa mnada nchini Namibia kwa kile kilichobainishwa kuwa ni adha ya kuongezeka kwa ukame huku kukishuhudiwa ongezeko kubwa la tembo nchini humo.

Hii sio mara ya kwanza Namibia inauza wanyama kwa mnada, ambapo msimu wa kiangazi inaelezwa kuwa kunatokea mgogoro kati ya wanyama na binadamu ambao ndio unaifanya Namibia kuuza tembo hao 170 kwa mnada.

“Kwasababu ya ukame na kuongezeka kwa idadi ya tembo, na mgogoro kati ya tembo na binadamu, kumetambulika haja ya kupunguza idadi ya wanyama hao”- kwa mujibu wa tangazo lililowekwa katika gazeti la New Era linalomilikiwa na serikali.

Tangazo hilo lililowekwa na wizara ya mazingira ni zabuni ya kutafuta kampuni inayofikia mahitaji yanayotakikana ikiwemo viwango vya kimataifa na kibali cha usafirishaji wa wanyama.

Mwaka jana, nchi hiyo iliidhinisha uuzaji wa karibu wanyama 1,000 ambao walikuwa katika hatari ya kufa kwasababu ya ukosefu wa chakula.

Aidha, wanyama waliokuwa wanauzwa ni pamoja na tembo, nyati, twiga na pala lengo likiwa ni kupatikana kwa dola milioni 1.1 kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.