Star Tv

Kundi la Taliban na serikali ya Afghanistan wanatarajia kuanza mazungumzo ya moja kwa moja ya amani Jumamosi, Septemba 12 huko Doha, nchini Qatar.

Mazungumzo hayo, yaliyocheleweshwa kwa zaidi ya miezi sita, yanatarajiwa kujaribu kumaliza karibu miaka 19 ya mgogoro kati ya pande hizo mbili hasimu nchini Afghanistan.

Chanzo cha serikali kimeliambia shirika la habari la AFP kuwa "Labda kujitokeze matatizo katika dakika za mwisho, timu ya (mazungumzo) ya serikali itaondoka kwenda Doha kesho, na tuna imani kuwa mazungumzo yatafanyika hivi karibuni, labda Jumamosi,".

Ikulu ya Rais nchini Afghanistan imeandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, kwamba ujumbe wake wa watu 21 utaondoka kwenda Doha leo Ijumaa.

Kwa upande wa kundi la Taliban wametangaza kuwa wako tayari kushiriki mazungumzo hayo na wamesisitiza juu ya nia yao ya kuendeleza mchakato wa mazungumzo pamoja na kuleta amani kamili na mfumo safi wa Kiislam ndani ya mfumo wa maadili yao ya Kiislamu na masilahi yao ya kitaifa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.