Mkutano wa pili wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS, unafanyika leo Ijumaa Agosti 28082020 tangu kufanyika kwa mapinduzi nchini Mali.
Tangu wiki iliyopita kundi la jeshi linaloshikilia madaraka limeendelea kupata shinikizo ili kurejesha taasisi za kiraia zilizochaguliwa.
Wiki iliyopita Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS ililita jeshi kumrejesha madarakani Ibrahim Boubacara Keita, na kuchukua uamuzi wa kufunga mipaka ya nchi wanachama jirani na Mali na kuiwekea nchi hiyo vikwazo vya kiuchumi. Lakini tangu wakati huo jeshi lilianza kulegeza msimamo wake. Jeshi lilikubali kumuachilia huru rais aliyepinduliwa Ibrahim Boubacar Keita.
Wakati huo huo mazungumzo kati ya wanajeshi wanaoshikilia madaraka nchini Mali na ECOWAS kuhusu uundwaji wa serikali ya mpitoa yameanza. Jumuiya hiyo imelitaka jeshi kuunda serikali ya mpito itakayoongoza nchi kwa mwaka mmoja.
ECOWAS "inakubali" wazo la "serikali ya mpito itakayoyoongozwa na raia au mwanajeshi mstaafu" kwa kipindi cha mpito cha "miezi sita, tisa, au kumi na mbili" nchini Mali, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi nchini humo, imesema taarifa kutoka ikulu ya rais wa Nigeria.
Taarifa hiyo ikimaanisha kuwa miezi hiyo waliyoitaja ni sawa na kipindi cha mwaka mmoja, huku jeshi la Mali likiwa linataka "kukaa madarakani" kwa "miaka mitatu" kabla ya kufanyika uchaguzi.