Star Tv

Katibu wa itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema amesikitishwa na kitendo kilichofanywa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) cha kuongeza ubeti katika wimbo wa taifa ambao waliimba katika kikao cha kumchagua mwanachama atakayepeperusha kijiti cha kuwania urais kupitia chama hicho.

Polepole ametoa kauli hiyo leo wakati alipofanya mkutano na waandishi wa habari na kusema kuwa kitendo hicho si cha busara kwa kuwa wimbo huo si wa chama chochote ni wa taifa hivyo unapaswa kutumiwa vyema na kuheshimiwa na watu wote pale unapoimbwa katika matukio mbalimbali.

Aidha, mbali na hilo Polepole amesema Chama Cha Mapinduzi Agosti 15, 2020 watazindua nyimbo zote ambazo nitatumia katika Kampeni mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru na amesema wasanii wote wa Bara na Visiwani mbalimbali watahudhuria haflahiyoi akiwemo Diamond, Harmonize watakuwepo.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bwana Polepole amesema mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama hicho atachukua fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo wiki hii jijini Dodoma ambapo amesisitiza kuwa siku ya kiongozi huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kuchukua fomu itatangazwa.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.