Star Tv

Serikali ya DRC yatangaza masharti mapya wakati wa mazishi nchini humo.

Hii ni kufuatia kuripotiwa kwa visa vya maambukizi ya corona nchini DRC, masharti mapya yametangazwa na serikali hasa kipindi cha mazishi ili kuepusha maambukizi zaidi.

Serikali ya nchini humo imetangaza kuwa watu wasiozidi ishirini ndio wataruhusiwa kuhudhuria mazishi, na atakayekiuka hatua hiyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Wakati huohuo maafisa wa afya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wamesema watu 400 waliokuwa wameambukizwa virusi vya Corona wamepona.

Kwa mujibu wa maafisa hao, watu zaidi ya elfu Mbili na mia nane wameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Covid-19, ambao umesababisha vifo vya watu 69.

Katika hatua nyingine, baadhi ya raia hawakupokea vizuri hatua ya serikali ambayo imetangaza utaratibu mpya wa mazishi hasa jijini Kinshasa huku waombolezaji wasiozidi 20 wakiruhusiwa kushiriki lengo likiwa ni kuepusha maambukizi zaidi.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.