Star Tv

Watu wenye Ualbino mkoani Mara wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa mafuta maalumu wanayotumia kupakaa ngozi zao ili kuepusha vidonda na michubuko ya ngozi inayosababishwa na mionzi ya jua hali inayopelekea baadhi yao kukumbwa na magongwa ya saratani ya ngozi.

Mionzi ya jua ni changamoto kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albinizim) ,kutokana na hali hiyo mafuta maalumu kwa ajili ya kupakaa ngozi zao ndio suruhisho la changamoto hiyo,ambapo watu hasa wanaoishi maeneo ya ijijini wanahitaji msaada huo ili kuepuka kukabiliwa na magonjwa ya saratani ya ngozi , mwenyekiti wa chama cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS)Tawi la Tarime Joseph Sinda amekiri kuwepo changamoto ya ukosefu wa mafuta hayo licha ya kuwepo kwa serikali na wadau mbalimbali kujitokeza na kuwasaidia . Pia Chama cha watu wenye ualbino wilaya Tarime kimetoa shukrani kwa serikali ya awamu ya tano kwa kuendelea kuwaamini na kuwateua watu wenye ualbino katika nafasi mbalimbali za uongozi ambapo wameomba jamii nayo kuwapa ushirikiano. Sinda ameiomba jamii kuacha kuwaamini waganga wa kienyeji wanaowaaminisha kwamba viungo vya mtu mwenye ualbino vinaleta utajiri.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.