Star Tv

Wizara ya afya nchini Uganda imethibitisha kifo cha mhudumu mwingine wa afya, ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatano.

Timu ya matabibu walipata virusi walipotibu mgonjwa wa kwanza aliyethibitishwa, ambaye alihitaji upasuaji, na wamelazwa katika hospitali ya mkoa ya Fort Portal.

Kwa mujibu na waziri wa afya Dkt. Jane Ruth Aceng amesema Margaret Nabisubi, mwenye umri wa miaka 58, anakuwa mhudumu wa afya wa nne kufa kwa Ebola.

Mwanafunzi wa udaktari Mtanzania, ambaye alikuwa sehemu ya timu hiyo, alifariki dunia mwishoni mwa juma. 

Aidha kuliliripotiwa kuwa mshukiwa wa kifo cha Ebola ambaye ni mkunga katika wilaya ya Mubende, ambaye aliaga dunia kabla ya kupimwa.

Wahudumu wa afya walikuwa wameelezea wasiwasi wao juu ya kutokuwa na vifaa vya kujilinda vya kutosha katika siku za kwanza za kuzuka kwa janga hilo.

Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa kumekuwa na kesi 43 zilizothibitishwa tangu kuzuka kwa ugonjwa huo kutangazwa wiki mbili zilizopita, na kumi kati yao wamekufa.

Maafisa wa afya walisema wamefuatilia zaidi ya watu 800 wanaoshukiwa kuwa walikutana na wale ambao wameambukizwa ugonjwa huo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.