Star Tv

Wizara ya afya nchini Uganda imethibitisha kifo cha mhudumu mwingine wa afya, ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatano.

Timu ya matabibu walipata virusi walipotibu mgonjwa wa kwanza aliyethibitishwa, ambaye alihitaji upasuaji, na wamelazwa katika hospitali ya mkoa ya Fort Portal.

Kwa mujibu na waziri wa afya Dkt. Jane Ruth Aceng amesema Margaret Nabisubi, mwenye umri wa miaka 58, anakuwa mhudumu wa afya wa nne kufa kwa Ebola.

Mwanafunzi wa udaktari Mtanzania, ambaye alikuwa sehemu ya timu hiyo, alifariki dunia mwishoni mwa juma. 

Aidha kuliliripotiwa kuwa mshukiwa wa kifo cha Ebola ambaye ni mkunga katika wilaya ya Mubende, ambaye aliaga dunia kabla ya kupimwa.

Wahudumu wa afya walikuwa wameelezea wasiwasi wao juu ya kutokuwa na vifaa vya kujilinda vya kutosha katika siku za kwanza za kuzuka kwa janga hilo.

Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa kumekuwa na kesi 43 zilizothibitishwa tangu kuzuka kwa ugonjwa huo kutangazwa wiki mbili zilizopita, na kumi kati yao wamekufa.

Maafisa wa afya walisema wamefuatilia zaidi ya watu 800 wanaoshukiwa kuwa walikutana na wale ambao wameambukizwa ugonjwa huo.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.