Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Dkt. Mpango amefanya mazungumzo na Guterres hayo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.
Aidha mara baada ya mazungumzo yao Makamu wa Rais amemkabidhi Guterres zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro unaopatikana hapa nchini Tanzania.
Leo Septemba 22, 2022 Makamu wa Rais akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuhutubia Mkutano wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaondelea nchini Marekani.