Star Tv

Baada kufanikiwa kupata ushindi wa ugenini na nyumbani katika michezo miwili ya ligi ya mabingwa Africa baadhi ya wadau wa soka wameuomba uongozi wa klabu ya Simba kuendelea kumuamini kocha wao wa muda Juma Mgunda.

Wadau mbalimbali wa soka wameongea juu ya suala hili, akiwemo Mchezaji wa zamani wa timu ya Kariakoo ya Lindi na mchambuzi wa soka Jemedari Said amesema uongozi wa klabu ya Simba unatakiwa kuendelea kumuamini Mgunda kutokana na mabadiliko ya kiuchezaji aliyoyafanya kwenye timu hiyo. Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu amesema wataendelea kuwa na kocha wao wa muda hadi pale uongozi wa klabu hiyo utakapotoa taarifa ya mabadiliko ya benchi la ufundi. Kocha wa muda wa klabu ya Simba Juma Mgunda ameiongoza timu hiyo katika michezo mitatu, mmoja wa ligi na miwili ya ligi ya mabingwa ambayo ameshinda michezo yote na kufunga mabao matano.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.