Star Tv

Baada kufanikiwa kupata ushindi wa ugenini na nyumbani katika michezo miwili ya ligi ya mabingwa Africa baadhi ya wadau wa soka wameuomba uongozi wa klabu ya Simba kuendelea kumuamini kocha wao wa muda Juma Mgunda.

Wadau mbalimbali wa soka wameongea juu ya suala hili, akiwemo Mchezaji wa zamani wa timu ya Kariakoo ya Lindi na mchambuzi wa soka Jemedari Said amesema uongozi wa klabu ya Simba unatakiwa kuendelea kumuamini Mgunda kutokana na mabadiliko ya kiuchezaji aliyoyafanya kwenye timu hiyo. Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu amesema wataendelea kuwa na kocha wao wa muda hadi pale uongozi wa klabu hiyo utakapotoa taarifa ya mabadiliko ya benchi la ufundi. Kocha wa muda wa klabu ya Simba Juma Mgunda ameiongoza timu hiyo katika michezo mitatu, mmoja wa ligi na miwili ya ligi ya mabingwa ambayo ameshinda michezo yote na kufunga mabao matano.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.