Star Tv

Kifo cha mhamiaji aliyeshambuliwa mchana kweupe nchini Italia kimezua hasira.

Shambulio dhidi ya mfanyabiashara huyo raia wa Nigeria lililotekelezwa mtaani na mwanamume mwingine katika kituo cha mji wa Civitanova Marche lilinaswa kwenye video siku ya Ijumaa.

Video hiyo, iliyochukuliwa na watazamaji bila jaribio lolote la kuingilia kati, inaonyesha mwathirika akiwa ameshikiliwa chini na raia mmoja mzungu.

Muitaliano mwenye umri wa miaka 32 amekamatwa kwa tuhuma za mauaji na wizi na mwathiriwa amejulikana kwa jina la Alika Ogorchukwu, baba aliyeoa na mwenye watoto wawili.

Mke wake, aliyetajwa kwa jina la Charity Oriachi, alishindwa kuzuia machozi yake alipokuwa akiviambia vyombo vya habari jinsi alivyoonyeshwa mwili wa mumewe ukiwa umelala chini.

Siku ya Jumamosi mamia ya watu kutoka jamii ya eneo la Nigeria waliingia katika mitaa ya Civitanova Marche, katika mkoa wa Marche, kudai haki huku shambulio hilo likilaaniwa na wanasiasa wa Italia.

#ChanzoBBC

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.