Star Tv

Kifo cha mhamiaji aliyeshambuliwa mchana kweupe nchini Italia kimezua hasira.

Shambulio dhidi ya mfanyabiashara huyo raia wa Nigeria lililotekelezwa mtaani na mwanamume mwingine katika kituo cha mji wa Civitanova Marche lilinaswa kwenye video siku ya Ijumaa.

Video hiyo, iliyochukuliwa na watazamaji bila jaribio lolote la kuingilia kati, inaonyesha mwathirika akiwa ameshikiliwa chini na raia mmoja mzungu.

Muitaliano mwenye umri wa miaka 32 amekamatwa kwa tuhuma za mauaji na wizi na mwathiriwa amejulikana kwa jina la Alika Ogorchukwu, baba aliyeoa na mwenye watoto wawili.

Mke wake, aliyetajwa kwa jina la Charity Oriachi, alishindwa kuzuia machozi yake alipokuwa akiviambia vyombo vya habari jinsi alivyoonyeshwa mwili wa mumewe ukiwa umelala chini.

Siku ya Jumamosi mamia ya watu kutoka jamii ya eneo la Nigeria waliingia katika mitaa ya Civitanova Marche, katika mkoa wa Marche, kudai haki huku shambulio hilo likilaaniwa na wanasiasa wa Italia.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.