Star Tv

Ukraine imethibitisha kwamba mamia ya wapiganaji wake waliokuwa wamekwama kwa zaidi ya miezi miwili katika mji wa Mauripol wameokolewa.

Naibu waziri wa ulinzi Hanna Maliar amesema kuwa wanajeshi walioumia vibaya 53 walipelekwa katika mji wa Novoazovsk, unaoshikiliwa na Urusi.

Hanna amesema kuwa wengine 211 walikombolewa kwa kutumia njia za kibinadamu kuelekea Olenivka mji mwingine unaodhibitiwa na waasi.

Awali Urusi ilisema mkataba umefikiwa wa kuwakomboa wanajeshi waliojeruhiwa.

Shirika la Habari la Reuters limeripoti kwamba takriban basi kumi na mbili zilizowabeba wapiganaji wa Ukraine waliokuwa wamekwama katika kiwanda kilichozingirwa zilionekana zikiondoka kusini mwa mji huo wa bandari jana Jumatatu jioni.

#ChanzoReuters
#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.